Sunday, March 11, 2012

SAFARI YA CCM KUVISAKA VITI VYAKE YAANZA KWA KISHINDO MWANZA.

"Nichagulieni jembe hili linalofiti viganja vyangu" Spika wa zamani wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Samweli Sita akimnadi kwa wananchi bw. Jack Masamaki kwa wananchi wa Kirumba Mwanza kwaajili ya kinyang'anyiro cha kiti cha udiwani kata hiyo.
Mpiganaji Jack 'Masamaki' kupitia tiketi ya CCM, alimwaga sera kwa wananchi wa kata yake kisha akapata nafasi ya kuomba kura.
Sehemu ya umati uliofurika kwenye uwanja wa Magomeni Kirumba katika mkutano wa hadhara wa kwanza wa kumnadi mgombea wa kiti cha udiwani kata ya Kirumba Mwanza, uchaguzi huu unafanyika kufuatia kifo cha aliyekuwa diwani ya kata hiyo marehemu Novatus Manoko.
"Mexico wamemudu sana ujenzi wa barabara sehemu za milima uko mkakati kuwawezesha madiwani wa Mwanza kufanya ziara wakaone ni jinsi gani wataboresha barabara sehemu za milima, wajifunze njia nyepesi za ujenzi wa barabara katika maeneo yote yanayopitika kwa tabu hivyo ndugu yangu Magufuli ajiandae kwani tunakwenda kushikamana" alisema Mh Samweli Sita
'Kubaliko' kwa vijana.
Mh. Sita akishuka jukwaani na Jack Masamaki kuanza maandamano mara baada ya mkutano kumalizika.
Mh Sita -" Mie kifaa' Umeona mambo yangu jukwaani....???" Katibu wa CCM Mkoa wa Mwanza- Umetisha mheshimiwa...!!!
Kutoka kushoto meneja wa uwanja wa CCM Kirumba John Tegete, Mgombea udiwani Jack Masamaki na Mh. Sita.
Safari ikaanza kupita mitaani ambapo kituo cha mwisho ilikuwa ni ofisi za CCM kata ya Kirumba.
Akinamama walifunga vibwebwe kuhakikisha wanamuunga mkono mwana wao wa nyumbani kufanikisha adhma yake iliyo na nia njema kwa wakazi wa kata ya Kirumba.
Ngoma inogile.......
Salaaamu kwa wadau wa ukweli mitaa ya Kirumba Polisi.........
Msafara ulikatisha sokoni kwa mbwembwe ukitoa salamu kwa wapiga kura...