Tuesday, July 22, 2014

DKT. KAMANI AMUKUNA WAZIRI MKUU PINDA AMUUNGA MKONO KWA UJENZI WA KITUO CHA ALBINO.








NA PETER FABIAN,
BUSEGA.

MBUNGE wa Jimbo la Busega mkoani Simiyu Dkt Titus Kamani adhamiria kuokoa maisha ya walemavu wa ngozi (Albino) baada ya kusaidia ujenzi wa kituo cha watoto wenye ulemavu eneo la kijiji cha Bukungu jimboni humo.

Hatua hivyo inatokana na vitendo vya mauaji ya kikatili kwa Albino vinavyokuwa vinafanyika wilayani humo na kumsukuma Dtk.Kamani, kuanzisha ujenzi wa kituo hicho cha kulelea watoto wenye ulemavu huo.

Kituo hicho kinachojengwa Kijiji cha Lukungu, Kata ya Lamadi, kitakachokuwa na uwezo wa kuchukua watoto zaidi ya 100, kinataraji kugharimu zaidi ya sh Bilioni 1.5 hadi kukamilika kwake.

Mbunge katika juhudi zake hizo za kuokoa maisha ya walemavu hao, zimeungwa mkono na Waziri Mkuu Mizengo Pinda, ambaye ameatoa kwa kuunga mkono kwa kuchangia kiasi cha sh milioni 5 kwa ajili ya kuongeza kasi ya  ujenzi ambao tayari umeisha anza na unaendela na unatarajiwa kukam ilika Agosti mwaka kesho.

Akizungumza katika eneo la ujenzi huo ambao umefikia hatua ya msingi jana, Dk Kamani alisema hali hii imenisukuma kwa moyo wa dhati kuhakikisha ujenzi huu unakwenda kwa kasi “lakini vitu ambavyo navifikiria sana na ningependa niondoke madarakani nikiwa nimevikamilisha, ni pamoja na kituo hiki cha walemavu.”alisisitiza

Aidha aliongeza kuwa hapa sisikilizi la mtu lazima kituo hiki kiishe na sitaki kiwe cha ujanja ujanja, namshukuru sana mheshimiwa Waziri Mkuu ambaye pia ni mlezi wa walemavu hao kuguswa na jitihada zangu na kuniunga mkono kwa kunichangia sh Milioni 5 zilizotolewa na Waziri Mkuu Pinda .

Alieleza kwamba, amekuwa akijishughulisha na makundi yaliyosahaulika hasa ya watu wenye ulemavu wa ngozi ambao nao ni sehemu ya jamii hivyo kituo hicho pia kitalea watoto wenye ulemavu wa viungo na macho, anaomba taasisi mbalimbali, watu wenye uwezo na wananchi wa eneo hilo wamuunge mkono ikiwa pamoja na kuwa walinzi wa watoto hao.

“Kampuni ya saruji ya Twiga tayari imetupatia mifuko 600 ya saruji iliyoanzisha ujenzi huo, imepaswa kuwa mfano bora wa kuigwa na yeye binafsi anagharamia fedha za kulipa mafundi, uchoraji wa ramani na usajiri wa kituo hicho ambacho kitaitwa Mother Thereza Albinus Disability Hope Centre,”alisema

Kwa upande wake Mratibu wa Kituo hicho Moody Gimonge alisema kwamba, kitakapokamilika kitaanza kwa kuchukua walemavu wa wilaya ya Busega wanaolelewa katika vituo vya Shule ya Msingi Mwisenge mkoani Mara, Buhangija mkoani mkoani Shinyanga na katika sehemu nyingine za wilaya hiyo.

Mratibu huyo alieleza kwamba, anasikitishwa kuona watu wengi wanaanzisha vituo hivyo kwa ajili ya maslahi yao binafsi badala ya kuwa na dhamira ya dhati ya kuwasaidia walemavu hao kama Dk Kamani alivyo dhamiria na ni Mbunge anayetimiza ahadi yake ya kusaidia jamii ya walemavu wakiwemo Albino.

Wito wangu kwa jamii iondokane na imani za kishirikina na mira potofu kwamba viungo vya Albino vinaweza kumpatia mtu utajiri wakati familia zao zilizozaa watoto hao zikiwa bado maskini hivyo kuwajengea tu vituo haitatosha bali jamii ielimike na kuchukua jukumu la kuwalinda na kuto wanyanyapaa kwani ni sawa na binaadamu wengine.

WAZIRI ASEMA SHERIA HAIRUHUSU UVUVI WA SAMAKI WACHANGA, NYAVU HARAMU NA BIASHARA.

WAZIRI wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Titus Kamani amewaonya wananchi wanaovua na kufanya biashara ya samaki wadogo wasiotakiwa kuvuliwa , kuacha na hakutakuwa na huruma kwa watakaokamatwa kwa uhalifu huo.
Alisema kwamba wanaotengeneza, kuingiza na kuuza zana haramu za uvuvi, nao watachukuliwa hatua kali ikiwa ni pamoja na kuadhibiwa kwa mujibu wa sheria kwa kuwa serikali kupitia Wizara yake itaendelea kulinda rasilimali zilizopo kwenye Bahari, Maziwa, Mito na Mabwawa ambayo baadhi ya wananchi wanatumia zana hizo haramu kufanya vitendo vya uhalifu huo.
Dkt. Kamani alieleza kwamba Sekta ya Uvuvi nchini hawezi kuwaletea manufaa watanzania wa leo na kizazi kijacho, iwapo uvuvi haramu utaachwa uendelea hivyo serikali haitawavumilia, itaendelea kuwakamata na kuwafikisha kwenye mkondo wa sheria kwa kukiuka sheria ya Uvuvi endelevu ya mwaka 2002.
“Hata mfugaji huwezi kuendelea iwapo unachinja ndama, nawaomba wananchi muwe walinzi wa rasilimali za majini na zilizopo kwenye maliasili zetu, wafichueni wote wanaojihusisha na vitendo vya uvuvi haramu, uuzaji wa samaki wadogo na ujangiri.” Alisema Kamani wakati akihutubia wananchi wa kijiji cha Jisesa na Busami wilayani Busega mkaoni Simiyu juzi.
Mbunge huyo alieleza kwamba, sheria hiyo ya uvuvi pia hairuhusu mfanyabiashara yoyote kuingiza au kuuza nyavu zenye matundu yasiyotakiwa hivyo wauzaji wa nyavu, samaki na wavuvi haramu wote wanapaswa kukamatwa na kuchukuliwa hatua za kisheria.

Hata hivyo baadhi ya wananchi walisikika katika mikutano hiyo, wakilalamikia maafisa Uvuvi wa wilaya ya Busega wamekuwa wakiwakamata baadhi ya wafanyabiashara wa samaki wanaokutwa wakiwa na samaki wadogo na hivyo kumuomba Waziri huyo wasikamatwe kwa kuwa wao hawavui ama kutengeneza nyavu zilizo pigwa marifuku.

Wednesday, June 4, 2014

WAZIRI KAMANI AWATAKA WANANCHI WA JIMBO LA BUSEGA KUIPA KIPAUMBELE ELIMU YA MSINGI

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Dr. Titus Kamani akiweka jiwe la msingi katika jengo la Ofisi ya Halmashauri ya kijiji cha Shimanilwe wiayani Busega mkoani Simiyu.








Friday, January 31, 2014

ZIARA YA WAZIRI WA MAENDELEO YA MIFUGO NA UVUVI DR.TITUS KAMANI YABAINI CHANGAMOTO ZA VITENDEA KAZI KITUO CHA UTAFITI WA SAMAKI MWANZA.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Dr. Titus Kamani(kulia) akiwa na Mkurugenzi wa Kituo cha Utafiti wa Samaki kituo cha Mwanza  (TAFIRI) Dr. Robert Kayanda wakitazama jinsi hatua mbalimbali za utafiti zinavyofanyika ndani na nje ya ziwa.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Dr. Titus Kamani akishuka toka katika boti ya utafiti mara baada ya kuzugukia maeneo ya utafiti ziwa Victoria ambapo pia aliambatana na wadau wengine wa kitengo husika mkoa wa Mwanza..
Boti ya utafiti ikiwa na Mhe. Waziri pamoja na wadau wa utafiti.
Kituo cha Utafiti wa Samaki Tanzania kituo cha Mwanza bado kinakabiliwa na changamoto ya upungufu wa vitendea kwa baadhi ya boti zake hazijakarabatiwa kwa muda mrefu na moja kati ya boti za utafiti imekufa injini yake ikihitaji kufufuliwa pamoja na changamoto ya bejeti finyu ya kuendeshea mradi. Mfano kwa mwaka jana Idara ya Uvuvi mkoa wa Mwanza iliiingizia serikali kiasi cha shilingi bilioni 3 lakini bajeti iliyopata haikuzidi shilingi milioni 12. 
"Serikali haito vumilia kuona uvuvi haramu ukiendelea kushamiri badala yake itaendelea kupambana kwa hali na mali na watu wanaotengeneza zana haramu za uvuvi ili kuwepo na uvuvi endelevu wenye tija kwa nchi yetu" 
PICHA NA ZEPHANIA MANDIA.
WA G. SENGO BLOG.

Saturday, January 25, 2014

DK KAMANI: AFUNGUKA, AWATAKA WAFANYAKAZI WASIOENDANA NA KASI YAKE WAJIONDOE MAPEMA


DK KAMANI: AFUNGUKA, AWATAKA WAFANYAKAZI WASIOENDANA NA KASI YAKE WAJIONDOE MAPEMA!

Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi Dr. Titus Kamani, amesema ili kwenda na kasi ya maboresho ya wizara hiyo, inahitajika dhana ya uwajibikaji na uwazi sambamba na kujitolea kwa nguvu zote katika kufanya kazi.

Waziri Kamani, ameyasema hayo leo katika mkutano wa kwanza uliowakutanisha wafanyakazi wote wa wizara hiyo, wakiwemo wastaafu wa mwaka jana katika ofisi za wizara hiyo zilizopo Temeke jijini Dar es Salaam.

Amesema kama kuna mtu ambaye ni kikwazo katika kukwamisha shughuli za wizara, ni bora akawapisha mapema na kwamba kila mtumishi kwa nafasi yake, anatakiwa kuifanya kazi kwa uwazi na akaitaka wizara kufanya kazi na vyombo vya habari kwani ndio njia pekee ya kuwafanya watanzania wajue wizara inafanya nini.

“Wewe upo ofisini, halafu unaogopa ogopa vyombo vya habari, kwani unatatizo gani, kuweni wazi mambo yenu yawe hadharani, watanzania wa Mbeya wayajue, Rufiji mpaka Pemba, hakuna kufichaficha jambo katika wizara yangu.” Alisistiza Dk Kamani.

Amesema wizara ya maendeleo ya mifugo na uvuvi ndio moyo wa taifa kwani huwajumuisha watanzania wengi wenye maisha ya kawaida, lakini amesikitishwa kwa jinsi ambavyo wizara hiyo imekuwa ikichukuliwa na baadhi ya watu kama ni wizara ya yenye migogoro na kuleta hasara maeneo mengine.

“N’gombe hawa wamekua wakiingia kwenye hifadhi, wanapigwa risasi, wanaaribu mashamba ya watu na kuleta njaa kwa wananchi, ngombe hawa wamekuwa wakiambiwa wanaleta uharibifu wa mazingira kwa wananchi kwa sababu ya kuhamahama, kama ngombe hawa ungepatikana utaratibu mzuri wa kuwatunza, kuwahifadhi basi, taifa hili lingeingiza kipato kikubwa ikiwemo kuuza nyama hadi nje ya nchi, maziwa na kuboresha afya za watanzania” alisema Dk Kamani.

Dk. Kamani, amesema anafahamu Wizara yake ina changamoto nyingi katika kutekeleza majukumu yake, ikiwemo bajeti kuwa ndogo, lakini kwa kutumia taaluma yake pamoja na ushirikiano wa wafanyakazi wote wa wizara hiyo, anaamini wizara hiyo badala ya kuonekana ni laana kwa watanzania, itakuwa ni wizara yenye neema kwa watanzania, yenye kueneza ajira na kipato kwa sababu hakuna jambo lisilowezekana kama kila mmoja atafanya kazi kwa dhamira moja.

Akizungumzia juu ya ranchi za taifa, waziri Kamani amesema ana nia ya dhati ya kuona ranchi za taifa zinafufuka na kutengeneza uchumi imara wa taifa, kuzalisha Ngombe wenye ubora ambao watatoa mazao ya mifugo yatakayoliingizia taifa hili kipato kikubwa.

Akizungumzia sekta ya uvuvi, Waziri Kamani, amesema sekta hiyo ni tabu tupu, amesema leo tunaambiwa kuna uvuvi haramu, nyavu zisizokidhi viwango, huku wavuvi wakiendelea kuwa masikini, katika nchi yenye bahari, maziwa na mito mikubwa kila kona, ameuliza ni kweli wanahitaji bajeti kubwa ya kushughulika na mambo hayo?.

“Tunahitaji utashi wa kuwasadia wavuvi wetu, kwa kutoa elimu na kufanya mazungumzo nao ya mara kwa mara, kuwatembelea maeneo yao ya kazi na kubaini matatizo yao kisha kuyafanyia kazi” Alibainisha Dk Kamani.

Kuhusu zao la kuku, Waziri Kamani amesema sasa hivi kuna tatizo la mayai feki na chanjo feki, alihoji ni kweli kwamba wafanyakazi wa wizara hiyo haiwajui wahusika au kuna baadhi ya watumishi ndio miradi yao? ambapo aliagiza wizara kubaini wanaofanya biashara hiyo feki ambayo inaleta madhara hasa wakazi wa mjini ambao ni watumiaji wakubwa wa bidhaa hizo.

Awali, kaimu katibu mkuu wa wizara hiyo Dk Yohana Budeba alipongeza uteuzi wa Dk Kamani, kuingia katika wizara hiyo kwakuwa ajira yake ya kwanza mwaka 1982  alikuwa chini ya wizara hiyo kama afisa Mifugo wa kata ya Kisongo wilaya ya Arumeru Mkoani Arusha, hivyo changamoto nyingi anazifahamu, ni mwenzao na anaamini watashirikiana vyema katika kukabiliana nazo.

Saturday, December 1, 2012

MH. WAZIRI MKUU PINDA NDIYE MGENI RASMI SERENGETI MARATHON ITAKAYO TIMUA VUMBI DEC 11/2012


Taasisi ya Serengeti Sports Centre ya jimbo la Busega mkoani Simiyu imeandaa mashindano ya mbio za nyika yatakayotambulika kama Serengeti Marathon yanayotaraji kuanza kutimua vumbi mnamo tarehe 11/12/2012.

Waziri mkuu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mizengo Kayanza Pinda anatarajiwa kuwa mgeni rasmi wa uzinduzi wa mashindano hayo ambayo si washiriki kutoka mkoa wa Simiyu pekee watashiriki, bali  pia Serengeti Marathon itashirikisha wafukuza upepo wa mikoa yote kwani tayari taarifa zimefika kwenye vilabu vya vyama vyote nchini vilevile balozi za nchi zote ukanda wa Maziwa Makuu na nchi zote za kimataifa zimepata mialiko, hivyo tutegemee kuona washiriki kutoka sehemu mbalimbali ulimwenguni.  

Bofya Play ili upate taarifa kamili, 

 
Zawadi kwa washindi wa michuano hiyo itakayoshirikisha makundi mawili yaliyotengwa kwa wanaume na wanawake wenye umri kuanzia miaka 18 na kuendelea:

Washindi wa kwanza shilingi.....500,000/=
Washindi wa pili shilingi .............400,000/=
Washindi wa tatu shilingi............300,000/=
Washindi wa nne shilingi............200,000/=
Washindi wa tano shilingi...........100,000/=
Nao Washindi wa 6 hadi 10 kwa kila upande (wanawake na wanaume)  kuondoka na kifutajasho cha shilingi 20,000/= kila mmoja....

Saturday, October 27, 2012

MBUNGE WA BUSEGA ATOA CHANGAMOTO KWA WAHITIMU WA KIDATO CHA NNE BADUGU

Mbunge wa Jimbo la Busega Dr. Titus Kamani ameataka wanafunzi 113 wa Shule ya Sekondari Badugu wajiendeleza zaidi ili wapate elimu ya juu itakayowawezesha kuwa wataalamu wa fani mbalimbali ili kuondoa umasikini na kuleta maendeleo endelevu.

Dr. kamani alitoa kauli hiyo hivi karibuni Katika maafali ya kidato cha nne katika shule hiyo, ambapo pia liwataka wahitimu hao kutoridhika na elimu ya kidato cha nne ambayo alisema kwa sasa ni ya chini mno kutokana na kukuwa kwa utandawazi na tekinolojia duniani.

Kabla ya mahafali hayo mbunge huyo alitembelea mradi wa jengo la maabara la shule ambalo limejengwa na wananchi pamoja na serikali kwa gharama ya zaidi ya shilingi milioni 20 ambapo yeye aliahidi kumalizia ujenzi huo kwa fedha kutoak mfuko wa jimbo.

Diwani wa kata hiyo Bw. James Yagaluka alimpongeza mbunge huyo na wazazi wa kata hiyo kwa kujitokeza kujenga sehemu ya jengo hilo la maabara na kuongeza kuwa nyumba mbili za waalimu zinajengwa kwa mpango huo.

Mkuu wa shule hiyo Bw. Isaack Tagaya ameiomba serikali kutakua haraka matatizo yanayoikabili shule hiyo yakiwemo ya ujenzi wa Hosteli ya wasichana ili kuepuka mimba kwa wasichana, uhaba wa maji, upungufu wa walimu na vitabu na ukosefu wa umeme.

Aidha mwalimu Tagaya alieleza mafanikio ya shule hiyo yakiwemo ya kutunza mazingira na usafi wa shule, wanafunzi kufanya vizuri katika mitihani mbalimbali, shule kuweza kufundisha masomo ya sayansi kwavitendo  na kudumisha michezo ambayo kwa sasa ni ajira na hujenga mwili.

Wanafunzi waliohitimu kidato cha nne shuleni  hapo katika risala yao walisema kuwa shule hiyo inakabiliwa na upungufu wa vyumba vya madarasa, walimu wa masomo ya sayansi na pia ukosefu wa vifaa vya michezo.