Thursday, December 29, 2011

MBUNGE WA BUSEGA Dk. TITUS KAMANI, AMEJIPANGA KUWATUMIKIA WANANCHI

Tuesday, May 3, 2011Makamu wa rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania na aliyekuwa mgombea mwenza wa urais wa CCM katika uchaguzi uliopita Dk. Mohamed Gharib Bilal, akisalimiana na wananchi wa Kijiji cha Lamadi eneo la Nyamikoma Wilaya ya Busega, wakati alipofika katika Jimbo la Busega kufanya mkutano wa kampeni na kumnadi mgombea ubunge wa jimbo hilo, Dk. Titus Kamani.

MBUNGE wa Busega Dk. Titus Kamani, amesema amejipanga kuhakikisha anawatumikia wananchi wake ili wapate maendeleo ya haraka.


Pia, amewashitakiwa kwa wananchi wake wanasiasa wanaompaka matope ikiwa ni mpango wa kuhakikisha anapoteza dira katika kutekeleza mipango ya maendeleo.


Hivi karibuni kumezuka kikundi cha wanasiasa waliokuwa wapinzani wa Dk. Kamani wakati wa mchakato wa kura za maoni, wakimpaka matope na kushawishi wananchi wasishiriki shughuli za maendeleo.


Akizungumza na mamia ya wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika Kata ya Nyashimo mjini Ramadi, juzi, ambapo alisema fitina zinazopikwa dhidi yake ni uendelezaji wa siasa chafu unaofanywa na wanasiasa wasiokubali matokeo.


Awali, kabla ya kuzungumza kwenye mkutano wa hadhara, mamia ya wananchi walijitokeza kumlaki Dk. Kamani wakati alipowasili mjini Ramadi pamoja na kumpongeza kwa kuchaguliwa Mwakilishi katika Bunge la SADC.


Alisema kuwa mikakati inayofanywa na wanasiasa kuhakikisha wanampaka matope kwa lengo la kumharibia sifa yake, si jambo zuri na halina budi kukemewa na wananchi wote wa Busega.


Hata hivyo, alisema kuwa hana muda wa kubishana na wanasiasa hao kwa kuwa uchaguzi ulishamalizika na kwamba, amejielekeza zaidi katika kuwatumikia wananchi wake na si kuendesha siasa za majitaka.


Aliwaasa wananchi kutokubali kurubuniwa na wanasiasa, ambao wana lengo la kuhakikisha wanakwamisha maendeleo jimboni humo ili kutaka kuonyesha kuwa hajawafanyia mambo mema wananchi wake.


Dk. Kamani alitumia fursa hiyo kuwaomba viongozi wa CCM kumlinda dhidi ya siasa chafu zinazoendeshwa dhidi yake na wanasiasa hao kwani, kwa sasa wamefikia hatua mbaya na isiyostahili kuvumiliwa. “Naomba CCM na viongozi wangu wanilinde juu ya mambo haya ninayofanyiwa… Nimeshinda kwa kura nyingi tena kwa kufuata taratibu zote na wananchi wamenikubali.


Kuanza kupakana matope kwa mambo mazito wakati uchaguzi ulishakwisha hakuna maana. Tushirikiane kukijenga Chama na kuwatumikia wananchi wetu. “Nimewaeleza haya wananchi wenzangu kwa kuwa ndiyo mlionipa hii nafasi ya kuwa mwakilishi wenu na mtaamua hatua za kuwachukuliwa hawa watu. Naomba muwaadhibu kwa kuwaeleza kuwa juu ya siasa chafu wanazonifanyia kuwa mmewabaini,” alisema Dk. Kamani.


Kuhusu kuchaguliwa mwakilishi wa Bunge la Tanzania katika SADC, Dk. Kamani alisema kumetokana na baraka alizopewa na wananchi wa Busega hivyo, atawatumikia mahali popote na muda wowote.

No comments:

Post a Comment