Thursday, January 5, 2012

UFUGAJI NYUKI NA UTUNZAJI MAZINGIRA

Ufugaji nyuki
1. Kuleta waelimishaji wa ufugaji nyuki toka TAWIRI/SIDO/Idara ya Misitu na Nyuki.
2. Kuanzisha vikundi vya ufugaji nyuki Badugu, Nyaluhande, Ngasamo, Kiloleli, Mwamanyili, Kabita, Shigala, Igalukilo, Malili, Mkula na Kalemela.
3. Kujifunza na kusindika mazao ya nyuki.
4. Kubaini na kuvutia masoko ya mazao ya nyuki (mf. Mohamed Enterprises kwa ajili ya nta).

Mazingira
1. Kuhamasisha upandaji miti kama zao la biashara – kwa familia na taasisi (kushirikiana na Tanzania Tree Seed Agency – TTSA, SUA, Chuo cha Olmotonyi na NGOs mf. Acord, Lake Victoria Environment Management Programme – LVEMP).
2. Kuanzisha miradi ya vitalu vya miti kibiashara – kwa taasisi na watu binafsi kwa kata na vijiji.
3. Kuhamasisha na kuwawezesha vijana waliomaliza mafunzo kwenye vituo vya ufundi (vocational training) kuanzisha miradi ya ufundi ya kuongeza thamani ya mazao ya miti.

No comments:

Post a Comment